SEKRETARIETI YA HALMASHAURI KUU YA CCM YA TAIFA
Sekretarieti ya Halmashauri Kuu ya CCM ya Taifa ina wajumbe wafuatao:-
i. Katibu Mkuu wa CCM ambaye atakuwa Mwenyekiti.
ii. Manaibu Katibu Mkuu wa CCM.
iii. Katibu wa Halmashauri Kuu ya Taifa wa Organaizesheni.
iv. Katibu wa Halmashauri Kuu ya Taifa wa Itikadi na Uenezi.
v. Katibu wa Halmashauri Kuu ya Taifa wa Mambo ya Siasa na Uhusiano wa Kimataifa.
vi. Katibu wa Halmashauri Kuu ya Taifa wa Uchumi na Fedha.
vii. Makatibu Wakuu wa Jumuiya za Wananchi zinazoongozwa na CCM.
Majukumu ya Sekretarietiya Halmashauri Kuu ya Taifa ni:-
· Kusimamia shughuli zote za utendaji za Chama kitaifa.
· Kuandaa shughuli za vikao vya Chama ngazi ya Taifa.
Majukumu ya Sekretarieti ya Halmashauri Kuu ya Taifa yanagawanyika ifuatavyo:-
(a) Katibu Mkuu wa CCM.
(b) Idara ya Organaizesheni.
(c) Idara ya Itikadi na Uenezi.
(d) Idara ya Mambo ya Siasa na Uhusiano wa Kimataifa.
(e) Idara ya Uchumi na Fedha.
Kila Idara inaongozwa na Katibu wa Halmashauri Kuu ya Taifa ya CCM. Idara ya Utawala na Uendeshaji Bara au Zanzibar inaongozwa na Naibu Katibu Mkuu wa CCM
Kila Idara ya Makao Makuu ya Chama inakuwa na Kamati ya Ushauri yenye Wajumbe wasiozidi watano akiwemo na Katibu wa Halmashauri Kuu ya Taifa.Wajumbe hao watateuliwa na Kamati Kuu ya Halmashauri Kuu ya CCM ya Taifa.
Habari Zaidi: |
||




