What's New
Speeches
Mkereketwa
Official Policy Documents
Official Working Documents





Mkutano Mkuu wa CCM wa Taifa




Mkutano Mkuu wa CCM wa Taifa ndicho Kikao Kikuu cha CCM kupita vyote na ndicho  kina  madaraka  ya  mwisho.

 


Mkutano Mkuu wa CCM wa Taifa unafanya mikutano yake ya kawaida mara tatu katika kipindi cha miaka mitano.   Mikutano miwili kati ya hiyo ni ya uchaguzi na mmoja ni wa kazi. Kalenda ya vikao vya Chama inaonyesha  ni  lini  mikutano  hiyo  mitatu itafanyika.  Lakini  mkutano  usiokuwa  wa kawaida unaweza kufanyika wakati wowote ukiitwa na Mwenyekiti wa CCM au ukiombwa na  theluthi  mbili  ya  wajumbe  wote  wa Halmashauri Kuu ya CCM ya Taifa.

Mkutano Mkuu wa CCM wa Taifa unaundwa na wajumbe wafuatao:-

i.            Mwenyekiti wa CCM.

ii.            Rais na Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania wanaotokana na CCM.

iii.            Makamu  wawili  wa  Mwenyekiti  wa CCM.

iv.            Rais wa Zanzibar anayetokana na CCM.

v.            Katibu Mkuu wa CCM.

vi.            Manaibu Katibu Mkuu wa CCM.

vii.            Katibu wa Halmashauri Kuu ya Taifa wa Organaizesheni.

viii.            Katibu wa Halmashauri Kuu ya Taifa wa Itikadi na Uenezi.

ix.            Katibu wa Halmashauri Kuu ya Taifa wa Mambo ya Siasa na Uhusiano wa Kimataifa.

x.            Katibu wa Halmashauri Kuu ya Taifa wa Uchumi na Fedha.

xi.            Wajumbe wote wa Halmashauri Kuu ya CCM ya Taifa.

xii.            Wabunge wote wanaotokana na CCM au kama Bunge limevunjwa wale wanachama wote waliokuwa Wabunge mara kabla ya kuvunjwa Bunge.

xiii.            Wajumbe wote wa Baraza la Wawakilishi wanaotokana na CCM au kama Baraza hilo limevunjwa wale wanachama wote waliokuwa  Wajumbe  wa  Baraza  la Wawakilishi mara kabla ya kuvunjwa kwa Baraza hilo.

xiv.            Makatibu wa Siasa na Uenezi wote wa Mikoa.

xv.            Makatibu wa Uchumi na Fedha wote wa Mikoa

xvi.            Wenyeviti wote wa CCM wa Wilaya.

xvii.            Makatibu wote wa CCM wa Wilaya.

xviii.            Makatibu wote wa Siasa na Uenezi wa Wilaya.

xix.            Makatibu wote wa Uchumi na Fedha wa Wilaya.

xx.            Mwenyekiti  na  Katibu  wa  Kamati  ya Wabunge wote wa CCM.

xxi.             Mwenyekiti  na  Katibu  wa  Kamati  ya Wajumbe wote wa Baraza la Wawakilishi wanaotokana na CCM.

xxii.             Mwenyekiti,  Katibu  Mkuu  na  Makamu Mwenyekiti  kutoka  kila  Jumuiya  ya Wananchi inayoongozwa au iliyojishirikisha na CCM ambao ni wana-CCM.

xiii.            Wajumbe  watano  waliochaguliwa  na Mkutano Mkuu wa CCM wa kila Wilaya.

x.         Mwenyekiti, Katibu wa Mkoa na Mjumbe mwingine mmoja aliyechaguliwa kutoka kila Mkoa wa Bara na Zanzibar kwa kila Jumuiya ya wananchi

 

 

   

   

Habari Zaidi:

   
     

ccm flag



Email
Links
Contact Us
CCM Creed   Conditions for Membership   Aim and Objectives

Chama Cha Mapinduzi believes that all human beings are equal

 

It is easy to be a member of CCM as its conditions for membership are directed towards an integrity citizen

 

CCM aims at defending the independence of our country and the freedom of its citizens

© COPYRIGHT 2002-2010
CHAMA CHA MAPINDUZI (CCM)
P.O. BOX 50, DODOMA - TANZANIA [TELEFAX: +255-22-2185245; EMAIL: katibumkuu@ccmtz.org]