What's New
Speeches
Mkereketwa
Official Policy Documents
Official Working Documents


KAMATI KUU YA HALMASHAURI KUU YA TAIFA YA CHAMA CHA MAPINDUZI



Waraka
 

Kazi za Kamati Kuu ya Halmashauri Kuu ya CCM ya Taifa ni:

(1)   Kutoa uongozi wa Siasa katika nchi.nn

(2)   Kusimamia utekelezaji wa shughuli za kila siku za CCM.

(3)   Kueneza Itikadi na Siasa ya CCM nchini.

(4)   Kusimamia  kampeni  za  Uchaguzi  na kampeni nyinginezo.

(5)   Kuteua Makatibu wa CCM wa Wilaya,Katibu wa Sekretarieti ya Halmashauri Kuu ya  CCM  ya  Taifa,  Makatibu  Wasaidizi Wakuu wa Idara na Wakuu wa Vitengo vya Makao Makuu ya Chama.

(6)   Unapofika  wakati  wa  Uchaguzi  Kamati Kuu ya Halmashauri Kuu ya CCM ya Taifa inashughulikia mambo yafuatayo:-

(a)  Kufikiria na kutoa mapendekezo kwa Halmashauri Kuu ya CCM ya Taifa juu ya Wanachama watakaosimama katika uchaguzi wa Mwenyekiti wa CCM.

(b)   Kufikiria na kutoa mapendekezo yake kwa  Halmashauri  Kuu  ya  CCM  ya Taifa  juu  majina  ya  Wanachama wasiozidiwatano    wanaoomba kugombea kiti cha Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.

(c)   Kufikiria na kutoa mapendekezo yake kwa Halmashauri Kuu ya CCM ya Taifa juu  ya  Wanachama  watakaosimama katika  uchaguzi  wa  Makamu  wa Mwenyekiti wa CCM.

(d)  Kufikiria na kutoa mapendekezo yake kwa  Halmashauri  Kuu  ya  CCM  ya Taifa juu ya majina ya Wanachama wasiozidi watatu ambao wanaomba kugombea kiti cha Rais wa Zanzibar.

(e)   Kufikiria na kutoa mapendekezo yake kwa  Halmashauri  Kuu  ya  CCM  ya Taifa juu ya Wanachama wanaoomba nafasi za uongozi katika CCM ambao uteuzi wao wa mwisho unafanywa na Halmashauri Kuu ya CCM ya Taifa.

(f)     Kufikiria na kutoa mapendekezo yake kwa  Halmashauri  Kuu  ya  CCM  ya Taifa juu ya Wanachama wanaoomba nafasi  ya  Ubunge  na  Wanachama wanaoomba  nafasi  ya  Ujumbe  wa Baraza la Wawakilishi.

(g)   Kufikiria na kutoa mapendekezo yake kwa Halmashauri Kuu ya Taifa juu ya Wanachama  wa  CCM  wanaoomba nafasi za uongozi katika Jumuiya za Wananchi zinazoongozwa na CCM, ngazi  ya  Mkoa  na  Taifa,  ambazo uteuzi wake wa mwisho hufanywa na Halmashauri Kuu ya CCM Taifa.

(7)   Kumsimamisha  uongozi  kiongozi  yeyote isipokuwa  Mwenyekiti  wa  CCM  na Makamu wa Mwenyekiti wa CCM endapo itaridhika  kwamba  tabia  na  mwenendo wake vinamwondolea sifa za uongozi.

(8)   Kuona  kwamba  masuala  ya  Ulinzi  na Usalama   wa   Taifa   na   Maendeleo yanazingatiwa.

(9)   Kuandaa mikutano ya Halmashauri Kuu ya\CCM ya Taifa.

(10)  Kuwa na mikakati endelevu ya kuimarisha Chama kimapato, kudhibiti mapato na mali za  Chama  na  kuthibitisha  matumizi  ya Chama katika ngazi ya Taifa.

   


   

Habari Zaidi:

   
     

ccm flag



Email
Links
Contact Us
CCM Creed   Conditions for Membership   Aim and Objectives

Chama Cha Mapinduzi believes that all human beings are equal

 

It is easy to be a member of CCM as its conditions for membership are directed towards an integrity citizen

 

CCM aims at defending the independence of our country and the freedom of its citizens

© COPYRIGHT 2002-2010
CHAMA CHA MAPINDUZI (CCM)
P.O. BOX 50, DODOMA - TANZANIA [TELEFAX: +255-22-2185245; EMAIL: katibumkuu@ccmtz.org]